NINI UFANYE ILI NYWELE ZAKO ZIKUE VIZURI?

🧚‍♀️Kwanza kabisa unapaswa kuzikubali nywele zako na kuzipenda , jambo hilo litapelekea mahusiano mazuri, kuelewa tatizo la nywele zako na kuanza kuchukua hatua taratibu ya kuzipatia uvumbuzi tatizo hilo.
🧚‍♀️Pili, unapaswa kufanya usafi wa kina wa ngozi na nywele zenyewe kwasababu endapo nywele zitaachwa chafu, basi ule uchafu unaziba matundu ya nywele na kuzuia njia kama vile ambavyo matundu ya uso yakiziba unapata chunusi.
🧚‍♀️Tatu, ni kulinda unyevu wa nywele. Pale nywele  zinapooshwa, yale mafuta asilia ya kuzilinda huondoka na uchafu. Nywele inabaki ikiwa na udhaifu fulani maana haiwezi hata kushikilia hayo maji yaliyoo vizuri na zikikauka zinakuwa kavu sana. Ni vizuri kabla hazijakauka vizuri, zikafanyiwa ‘condition’ , kwa zile nywele ambazo ni nyepesi na chache pia kuna bidhaa zinasaidia kutunza vizuri unyevu na hivyo kuwa na afya nzuri.
🧚🏻‍♂️Hatua inayofuata ni ya kupaka mafuta kichwani, kwani mafuta yana umuhimu mno katika ukuaji wa nywele na mafuta mazuri ni ya kimiminika kama vile Black castor oil, Coconut oil, Jojoba oil nk  ambayo yamewafaa baadhi ya watumiaji wengi .
🧚🏻‍♂️Njia nyingine ni ya kuzichambua vizuri nywele kabla ya kuzichana, hapa mtu anatakiwa kuwa na subira na nywele zake , asifanye haraka haraka kuzichana na ikiwezekana aziloweshe maji kidogo halafu ndipo azichane kwa chanuo kubwa lenye upana wa kutosha (wide toothed comb) ili kuzipa afya na kuepuka kujiumiza wakati wa kuzichana.
NB: Mtu anayetunza nywele za asili anatakiwa kupunguza matumizi ya moto kama vile pasi ya nywele, dryers na vingine kama hivyo. Nywele zinatakiwa zichanwe kawaida na ziachwe zikauke zenyewe kwa hewa bila kuzilazimisha.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad