MAKOSA UNAYOFANYA WAKATI WA KUOSHA NYWELE ZAKO- PART 2



🧚🏻‍♂️Kutokuosha na kurudiaRinse & Repeat

Ni muhimu sana kuosha nywele na kurudia. Na hii ni muhimu zaidi kwa wale wenye nywele ndefu. Kama una nywele fupi au ndogo kabisa si lazima kwako kuosha na kurudia. Baada ya kuwa umesugua ngozi ya kichwa “scalp” kwa dakika tatu, ni muda wa kuosha nywele. Ukishaosha inafuata hatua ya pili ya uoshaji wa nywele. Unatumia shampoo kama kawaida. Kwenye hatua hii utaweka msisitizo zaidi kwenye nywele zenyewe kwakuwa tayari ngozi ya kichwa ulishashughulika nayo kabla. Mara hii weka msisitizo zaidi kwenye kuosha nywele zako na hakikisha hakuna nywele inayoachwa bila kupata shampoo kuanzia kwenye mzizi mpaka kwenye ncha.
🧚🏻‍♂️Kutokutoa  shampoo vizuri kwenye nywele.
Baada ya kurudia kuosha nywele kwa mara ya pili kinachofuata ni kutoa shampoo kwenye nywele.
Watu wengi hawatoi shampoo vizuri kwenye nywele, na hii huzifanya nywele kubaki na shampoo ambazo zinasababisha nywele kubaki na vitu vyeupe vyeupe “build-ups” na nywele pia kutosafishika vizuri. Hivyo inasisitizwa kutumia muda na maji ya kutosha kutoa shampoo na kuhakikisha imetoka kabisa kwenye nywele ili nywele zako ziwe zimesafishika vizuri.
Yapo makosa mengi sana ya utunzaji wa nywele yakianziwa na uoshaji wa nywele. Ila tukianza kuyasahihisha baadhi ya makosa tuliyoyaelezea hapo juu na kuanza kufuata utaratibu mzuri wa uoshaji wa nywele naamini sote tutakuwa tumeanza safari nzuri ya kuelekea kuwa na nywele nzuri na zenye afya!
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad