JINSI YA KUTUNZA NGOZI YA KICHWA

Mara nyingi tumekua tumeongelea jinsi ya kutunza nywele, leo tutaangalia  jinsi ya kuwa na ngozi ya kichwa yenye afya (Healthy Scalp)

🍀Nini ufanye ili uweze kumaintain ngozi yenye afya na kama ngozi yako ina afya ni rahisi nywele kuota vizuri na nywele kuwa na muonekano mzuri hivo msingi mzuri wa utunzaji wa nywele unaanzia kwenye ngozi yako  ya kichwa itunze vizuri sio kila mafuta unatumia unaharibu ngozi yako cha Kwanza,

NINI UFANYE
👉Kula vizuri na kunywa  maji kwa wingi
👉Epuka kuosha mara kwa mara nywele yako au mara chache wengine huosha mara moja hupelekea mrundikano wa uchafu.
👉Tumia  natural products (zisizo na viambata sumu) kwa nywele yako lakini pia unaponunua zingatia ingredients zillio tumika kutengenezea hizo products na muda wake wa kuisha (Expiry date)
👉Epuka  rangi za nywele na hata dawa za nywele zinadhoofisha sana nywele
👉Epuka  kusuka misuko hatarishi au kukazwa sana lakini pia massage kichwa chako mara kwa mara.


🍀Lakini pia kama unatatizo la miwasho mba wasioisha basi tumia steaming ya  tangawizi kitunguu swaumu na kitunguu maji saga pamoja unaweza changanya  na asali ukaweka kichwan kwa tumia hata mara 4 kwa miezi 2 (Hili somo lilishaelekezwa kwenye posts zilizopita👉🏻👉🏻

🍀Au unaweza kuoshea apple cider vinegar unachanganya na maji vijiko viwili vya maji kwa kimoja cha apple cider vinegar (Hili pia lilishaelezewa)

🍀Pia unaweza kuosha nywele ukakata mistari kisha ukascrub kichwa chako kisha ukaosha tena hapa nazungumzia scrub ya sukari ukachanganya na mafuta ya castor oil  au scrub ya sukari, kahawa na asali unachanganya kisha ukascrub kichwani ukimaliza iyache ikae hata dakika 5 kisha osha. Scrub ni nzuri sana maan itasugua vzr mba watoke na inatibu miwasho kwa haraka pia hii njia sio steaming kwa nywele zako hivo unaweza ukaamua ufanye lini na ukitumia hii njia utatakiwa kuweka tena steaming kama kawaida.
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad