JINSI YA KUREFUSHA NYWELE KWA HARAKA

Kama wewe ni mwafrika au una asili ya afrika basi tambua kuwa nywele zetu hukuckua muda mrefu sana kurefuka. Lakini zipo njia zinazo weza kukusaidia kurefusha nywele zako kwa haraka. Leo tujifunze kidogo njia mojawapo ya kukuza nywele zako kwa haraka zaidi.

NJIA YA KWANZA
Kuosha na matibabu.

-Tambua aina ya nywele zako
Unaweza kutambua aina ya nywele zako kwa kuwaona wataalamu wa saloon, kujua aina ya nywele zako itakusaidia kuchagua matibabu sahihi na products  sahihi kulingana na nywele zako.

-Osha nywele zako pale tu inapo hitajika.
Usipende kuosha nywele zako mara kwa mara kwani unaziondolea mafuta ya asili. jaribu kuosha nywele zako mara moja kwa wiki au mara moja kwa wiki 2 kama huwa zinakatika katika.Tumia  shampoo ambayo haita zaicha nywele zako zikiwa kavu sana. Ili kupunguza  madhara ya bidhaa unazotumia zioshe  nywele zako kwenye maji ya vuguvugu kisha zisuuze kwenye maji yaliyo poa.

-Ziache  nywele zako zikauke zenyewe
Kama unatumia hair blower kukaushia nywele zako ni vyema utambue kwamba joto kutoka katika blower linaweza kukusababishia madhara katika nywele zako na kuzifanya zikatike kabla hazijafikia urefu unao uhitaji. Badala  yake unaweza kuzikusanya nywele zako na kuzifunga kitambaa na uziache zikauke usiku kucha, Au unaweza kuzikausha kwa kutumia taulo.
-Tumia conditioner kila  unapo osha nywele zako.
Shampoo inaondoa mafuta ya asili yaliyopo kwenye nywele zetu, badala yake unaweza kurudisha mafuta hayo kwa kutumia conditioner inayo faa kulingana na nywele zako.

-Paka mafuta ya nywele kila siku.
Ukipaka mafuta ya nywele unazifanya nywele zako ziwe laini  hii itakusaidia kuzuia zisikatike.
Tumia mafuta ya maji (kimiminika) kama vile;
🧚🏻‍♂️ Black castor oil
🧚🏻‍♂️Lavender oil
🧚🏻‍♂️Avocado oil
🧚🏻‍♂️Olive oil
🧚🏻‍♂️Coconut oil nk
Zifunge  nywele zako na kitambaa kuzisaidia zishike mafuta.

ITAENDELEA......
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad