14. FAIDA ZA BAMIA KWENYE NYWELE

Bamia (okra) zinajulikana sana kama mboga na dawa kwa baadhi ya maradhi ya mwili lakini pia ni kiungo muhimu sana kwa ajili ya matunzo ya nywele na kukusaidia kupata nywele zenye afya nzuri zaidi.
Bamia zinaweza  kutumika kama:
🍃Leave in conditioner
🍃Steaming
🍃Kiungo cha kuondoa mba
🍃Kulainisha ngozi ya kichwa
🍃Kufanya nywele kuwa imara na rahisi kuzitunza
🍃Unaweza kutumia kusukia au kustyle nywele zako pia


Mahitaji
🍃Bamia kumi (10)
🍃Mafuta ya maji (African Black castor oil au coconut oil au olive oil)
🍃Juice ya Tangawizi
🍃Asali

Jinsi ya kuandaa
🌿Osha bamia zako vizuri kuondoa uchafu wote
🌿unaweza kukata kata kuwa vipande vidogo vidogo au ukamenya tu (kuexpose undani wake)
🌿Weka kwenye sufuria yako safi
🌿Ongeza maji kiasi (kikombe kimoja au viwili  vinatosha) na ufunike
🌿Chemsha kwa dakika 10 hadi 15 mpaka ile gelly au ute wa bamia uwe umetoka wa kutosha
🌿Epua na uache ipoe kwa dakika kadhaa
🌿Baada ya hapo chuja kuondoa vipeke na upate gelly tuu

Kama unatengeneza steaming
🌿chukua ute ulioupata gawanya mara mbili
🌿Nusu ya kwanza changanya na tangawizi na asali na mafuta yoyote ya kimiminika (hasa Castor oil)
🌿Baada ya kuosha nywele kwa shampoo (hakikisha nywele zako ni safi) paka mchanganyiko kwenye nywele zote
🌿Vaa shower cap au steamer na ukae kwa dakika 30+
🌿Osha kwa maji mengi
🌿Chukua ule mchanganyiko uliobaki changanya na mafuta kijiko kimoja hapa utakua umepata (Leave in Conditioner)
🌿Nywele zako zikiwa mbichi na safi pakaa vizuri kuanzia kwenye ngozi hadi kwenye ncha.
🌿Chambua vizuri nywele zako kidodgo kidogo kuhakikisha imeingia vizuri kwenywe nywele zote.
🌿Unaweza kusuka mabutu (bantu knots) au twists za njia mbili au tatu au nywele za mistari kawaida nywele lazima ziwe na unyevu  kabisa.
🌿Ukiona zinakauka unanyunyiza maji tena.
🌿Ukimaliza acha zikauke vizuri utaendelea kupaka mafuta yako kama kawaida ili kuzifanya zing’ae.
🌿Ukifumua unapata mawimbi mazuri unaweza kubana utakavyo nywele zako.

Faida zake
🍃Jelly ya bei rahisi kwa nywele za kuvutia
🍃Hutumia muda mchache kuandaa
🍃kirutubisho muhimu kwenye nywele
🍃kung’arisha nywele zako kama ilivyo kwa Alovera

NB: kwa wale wenye dawa unaweza kutumia kama leave in conditioner.
Pia ni nzuri sana kwa nywele za watoto maana haina kemikali.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad